VIDEO: BOSI SIMBA AMTAJA CLATOUS CHAMA/ JOSHUA MUTALE

AHMED Ally, Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano Simba SC ameweka wazi kuwa kiungo Joshua Mutale ambaye alicheza kwenye mchezo dhidi ya JKT Tanzania amerejea kwenye ubora ambao alikuwa nao muda mrefu lakini ulikuwa unakosekana.

Kwenye mchezo dhidi ya JKT Tanzania uliochezwa Mei 5 2025 alikuwa kwenye kiwango bora jambo lililochangia timu hiyo kupata ushindi wa bao 1-0 ambalo lilifungwa dakika ya 45 na kiungo Fabrince Ngoma.

Ahmed amemtaja kiungo wa zamani wa Simba SC ambaye kwa sasa yupo kwenye changamoto mpya ndani ya kikosi cha Yanga SC Clatous Chama.