SIMBA YATAMBIA UWEPO WA MWAMBA HUYU

UONGOZI wa Simba umetambia uwepo wa kinara wa kucheka na nyavu ndani ya Ligi Kuu Tanzania Bara ambayo ni namba nne kwa ubora, Jean Ahoua kwa msimu wa 2024/25 akiwa ni chaguo la kwanza la kocha.

Ndani ya kikosi cha Simba kiungo huyo rekodi zinaonyesha kuwa amecheza jumla ya mechi 21 akikomba dakika 1,550 na mguu wake wenye nguvu ni ule wa kulia kwa kuwa mabao yote aliyonayo kibindoni kafunga kwa kutumia mguu huo.

Ikumbukwe kwamba Ahoua ni mkali kwenye mapigo ya penati kwenye mabao aliyonayo ni matano alifunga kwa penati huku akindika rekodi yakufunga penati mbili kwenye mchezo dhidi ya Namungo uliochezwa Uwanja wa Majaliwa langoni alikuwa kipa Jonathan Nahima.

Ahoua ndani ya ligi katupia mabao 12 akiwa na pasi 7 za mabao hivyo kahusika kwenye mabao 19 kati ya 52 yaliyofungwa na Simba inayonolewa na Kocha Mkuu, Fadlu Davids ikiwa nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi.

Kwa mwendo alionao kwenye ligi anawastani wakuwa na hatari ndani ya uwanja kila baada ya dakika 81 anashikilia rekodi ya kuwa kiungo wa kwanza kutoa pasi ya bao ndani ya Simba ilikuwa kwenye mchezo dhidi ya Fountain Gate uliochezwa Uwanja wa KMC Complex alitoa pasi hiyo kwa Che Malone.

Ahmed Ally, Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano Simba amesema kuwa wachezaji waliopo ndani ya kikosi cha Simba wanatimiza majukumu yao kwa ushirikiano huku kiungo wao Jean Ahoua akizidi kuimarika taratibu kwa kuwa licha yakufunga mabao bado hajafikia kwenye viwango vya juu.

“Ahoua ni mashine ya kazi nah apo unaona kwa namna anavyotimiza majukumu yake bado hajafikia asilimia 100 ya ubora wake, kuna muda unakuja mzuri zaidi Wanasimba watafurahi kwani anajua mpira akiwa uwanjani, wengi wanasema hivi na vile lakini kijana yupo kwenye mwendo.

“Unamuona akiwa na mpira anakuwa na maamuzi halafu anafikiria ushindi bado kuna yale ambayo yanazungumzwa juu yake kazi inaendelea ni hakika furaha itakuwa kwa mashabiki wakipata burudani kutoka kwa mnyama, huu ni ubaya ubwela .”

Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo, kukipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371. Ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Moyo Wangu Unavuja Damu usipange kukosa.