>

AWESU AWESU, ONANA WAWASILI MISRI KWENYE KAMBI YA SIMBA

Wakati klabu ya KMC Fc ikiendelea kulalamika kuwa bado ina mkataba halali na Kiungo Awesu Ali Awesu, nyota huyo wa zamani wa Madini Fc tayari amewasili kwenye kambi ya Wekundu hao wa Msimbazi Nchini Misri kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya wa 2024/25.

Awesu ameambatana na Mshambuliaji Willy Essomba Onana kuungana na wachezaji wengine kwenye kambi hiyo iliyopo lsmailia, Misri.